Ajali ya barabarani yaua watu 27 nchini Kenya.

In Kimataifa

Polisi nchini Kenya wanasema kiasi ya watu 27 wameuawa hii leo baada ya basi la abiria kugongana na lori nchini humo.

Polisi wanasema tukio hilo limetokea katika barabara kuu inayounganisha miji miwili mikubwa nchini humo ya Nairobi na bandari ya Mombasa.

Leonard Kimaiyo ambaye ni mkuu wa polisi katika eneo la Kambu kwenye kaunti ya Makueni amesema basi hilo lilikuwa likielekea Mombasa na lori lilikuwa liielekea upande mwingine wakati ajali hiyo ilipotokea.

Ajali za barabarani zinaua takribani watu 3,000 nchini Kenya kila mwaka.

Vifo vitokanavyo na ajali za barabarani vimeongezeka nchini humo katika miaka ya karibuni licha ya hatua zinazochukuliwa dhidi ya madereva wanaoendesha magari wakiwa wamelewa ikiwa ni pamoja na kutozwa fani kali na vizuizi vya barabarani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu