Ajali ya barabarani yaua watu 27 nchini Kenya.

In Kimataifa

Polisi nchini Kenya wanasema kiasi ya watu 27 wameuawa hii leo baada ya basi la abiria kugongana na lori nchini humo.

Polisi wanasema tukio hilo limetokea katika barabara kuu inayounganisha miji miwili mikubwa nchini humo ya Nairobi na bandari ya Mombasa.

Leonard Kimaiyo ambaye ni mkuu wa polisi katika eneo la Kambu kwenye kaunti ya Makueni amesema basi hilo lilikuwa likielekea Mombasa na lori lilikuwa liielekea upande mwingine wakati ajali hiyo ilipotokea.

Ajali za barabarani zinaua takribani watu 3,000 nchini Kenya kila mwaka.

Vifo vitokanavyo na ajali za barabarani vimeongezeka nchini humo katika miaka ya karibuni licha ya hatua zinazochukuliwa dhidi ya madereva wanaoendesha magari wakiwa wamelewa ikiwa ni pamoja na kutozwa fani kali na vizuizi vya barabarani.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu