Ajib awataka mashabiki wawaunge mkono.

In Kitaifa, Michezo

Mchezaji wa Klabu ya Mabingwa watetezi wa Ligi kuu Bara Yanga SC Ibrahim Ajibu amesema matokeo yasiyoridhisha wanayoyapata hivi sasa, ni sehemu ya mchezo, hivyo mashabiki waendelee kuwaunga mkono.

“Mashabiki watulie na waendelee kutuunga mkono ili tuweze kufanya vizuri kwenye mechi zijazo kwa sababu haya matokeo hata sisi hatuyafurahii.

“Matokeo yetu dhidi ya Singida ni sehemu ya mchezo, tulijitahidi sana kuhakikisha tunapata ushindi lakini haikuwa hivyo kwa sababu na wenzetu nao walijipanga, kikubwa ifahamike wazi kwamba, ligi bado mbichi,” amesema Ajibu.

Yanga imepata sare ya pili mfululizo huku mashabiki wake wakionyesha kutofurahishwa baada ya kikosi chao kuomba mechi iishe mapema wakati Singida United walipokuwa wakishambulia kama nyuki.

Yanga na timu nyingine zina nafasi ya kujiandaa kwa kipindi hiki kutakuwa na mapumziko wakati wa kalenda ya Fifa, hivyo ni nafasi nyingine kuyafanyia kazi makosa ambayo yamekuwa yakijitokeza.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu