Jamaa mmoja wa umri 38, amewashangaza wanajamii wa kaunti
ya Kakamega nchni Kenya,baada ya kujichimbia kaburi na kisha
kujitoa uhai kwa kukunywa sumu.
Fred Luvale ambaye alikuwa utingo katika barabara ya Butali
kuelekea Webuye,anasemekana kufanya kitendo hicho baada ya
mama yake mzazi kumkataza kuuza kuku wake mwenyewe.
Luvale alitaka kuuza kuku hao ndipo awanunulie watoto wake
chakula lakini mama yake hakupendelea wazo hilo.
Marehemu anasemekana kugombana na mama yake kwa dakika
chache kabla ya kuamua kujiua.