Aliyekuwa kiongozi wa kundi la waasi la FPLC nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Bosco Ntaganda, hatimaye atatoa ushahidi wa kujitetea katika Mahakama ya Kimataifa ya ICC siku ya Jumatano.

In Kimataifa

Aliyekuwa kiongozi wa kundi la waasi la FPLC nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Bosco Ntaganda, hatimaye atatoa ushahidi wa kujitetea katika Mahakama ya Kimataifa ya ICC siku ya Jumatano.

Ntaganda maarufu kama “The Terminator” amekuwa akikanusha madai kuwa aliwatumia watoto wadogo kama wapiganaji na kuwatumia wanawake na wasichana kama watumwa wa kingono.

Kesi dhidi ya Ntanganda ilianza miaka miwili iliyopita mjini Hague, alipofunguliwa mashtaka ya mauaji katika jimbo la Ituri yaliyotokea kati ya mwaka 2002 na 2003.

Ntaganda mwenye umri wa miaka 43, amekanusha madai yote 13 ya uhalifu wa kivita na mengine matano ya ukiukwaji wa haki za binadamu, yaliyotekelezwa na waasi hao.

Watu zaidi ya 60,000 walipoteza maisha na wengine kuyakimbia makwao baada ya kuvamiwa na waasi hao.

Kabla ya kufikishwa katika Mahakama ya ICC, Ntaganda alijisalimisha katika Ubalozi wa Marekani jijini Kigali  nchini Rwanda mwaka 2013.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu