Amani Golugwa amesema kuwa hawaridhiki na mazingira ya madiwani wao saba kujivua nafasi zao za madaraka.

In Kitaifa

Katibu wa  Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Kaskazini, Aman Golugwa amesema kuwa hawaridhiki na mazingira ya madiwani wao saba kujivua nafasi zao za madaraka.

Ameyasema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari ambapo amesema kuwa sakata hilo wameamua kulifikisha kwa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ( Takukuru) na Tume ya Maadili ya Viongozi wa Umma ili iweze kutafutiwa ufumbuzi.

Amesema kuwa haoni sababu yeyote ya msingi ya viongozi hao kujivua nafasi zao ndio maana wamefikia hatua hiyo ya kulifikisha jambo hilo mbele ya vyombo hivyo ili viweze kulichunguza kiundani zaidi.

Hata hivyo, amewataka wafuasi wa Chama hicho kutotafuta mchawi bali wafukuze wasaliti waliomo ndani ili waweze kukijenga na kuimarisha utendaji kazi wake katika kutoa upinzani uliokuwa imara.

Hivi karibuni madiwani saba wamejivua uanachama wa chama hicho katika kata za Abureni, Ngabobo, Muriet, Legaruki, Makiba, Maroroni na mwingine ni wa diwani wa viti maalumu kutoka chama hicho.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu