Amnesty International limesema uchaguzi wa Rais wa Rwanda utakaofanyika mwezi ujao utafanyika katika mazingira ya hofu.

In Kimataifa

Shirika la kimataifa linalohusika na utetezi wa haki za binadamu la  Amnesty International limesema uchaguzi wa Rais wa Rwanda utakaofanyika mwezi ujao ambao pia Rais wa sasa Paul Kagame atakuwa anawania muhula wa tatu wa uongozi utafanyika katika mazingira ya hofu.

Kwa mujibu wa Amnesty uchaguzi huo utakaofanyika August .4 utafanyika huku kukiwa na rekodi kwa wanasiasa wa upinzani nchini humo kudhibitiwa, waandishi wa habari pamoja na wanaharakati kutiwa magerezani, kuuawa na wengine kulazimika kuikimbia nchi hiyo.

Rais wa Rwanda Paul Kagame amekuwa Rais wa nchi hiyo tangu wakati kundi lake la waasi lilipokomesha mauaji ya halaiki nchini humo ya mwaka 1994.

Hadi sasa ni mgombea mmoja tu wa upinzani , Frank Habineza aliyepitishwa na tume ya uchaguzi nchini humo kushindana na Rais Kagame katika uchaguzi huo. Wagombea wengine akiwemo mwanamke mmoja bado wanasubiri hatima yao ya kupitishwa na tume hiyo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu