Amnesty International limesema uchaguzi wa Rais wa Rwanda utakaofanyika mwezi ujao utafanyika katika mazingira ya hofu.

In Kimataifa

Shirika la kimataifa linalohusika na utetezi wa haki za binadamu la  Amnesty International limesema uchaguzi wa Rais wa Rwanda utakaofanyika mwezi ujao ambao pia Rais wa sasa Paul Kagame atakuwa anawania muhula wa tatu wa uongozi utafanyika katika mazingira ya hofu.

Kwa mujibu wa Amnesty uchaguzi huo utakaofanyika August .4 utafanyika huku kukiwa na rekodi kwa wanasiasa wa upinzani nchini humo kudhibitiwa, waandishi wa habari pamoja na wanaharakati kutiwa magerezani, kuuawa na wengine kulazimika kuikimbia nchi hiyo.

Rais wa Rwanda Paul Kagame amekuwa Rais wa nchi hiyo tangu wakati kundi lake la waasi lilipokomesha mauaji ya halaiki nchini humo ya mwaka 1994.

Hadi sasa ni mgombea mmoja tu wa upinzani , Frank Habineza aliyepitishwa na tume ya uchaguzi nchini humo kushindana na Rais Kagame katika uchaguzi huo. Wagombea wengine akiwemo mwanamke mmoja bado wanasubiri hatima yao ya kupitishwa na tume hiyo.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu