Babu Seya na Mwanaye Papii Kocha OUT!

In Kitaifa
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amri Jeshi Mkuu, ametangaza msamaha kwa Nguza Viking maarufu kama Babu Seya na mwanaye Jonson Nguza (Papii Kocha) ambao waliofungwa maisha katika Gereza la Ukonga jijini Dar es Salaam na kutaka waachiwe huru mara moja kutoka gerezani.
“Tanzania tuna jumla ya wafungwa 39,000 ambapo wanaume ni 37,000 na wanawake 2,000.  Wafungwa waliohukumiwa wako 522 kati yao wanaume ni 503 na wanawake ni 19. Nimeamua kusamehe wafungwa 8157, ambapo baada ya msamaha huu wafungwa 1828 watatoka leo.
“Mfano wa watu niliowasamehe ni Mzee Mganga Matonya mwenye umri wa miaka 85 amekaa Gerezani miaka 37 na miaka 7 ya kukaa mahabusu. Nimeamua kusaheme familia ya Nguza Viking jina lingine anaitwa Babu Seya na Ndugu Johnson Nguza ama Papii Kocha.
“Nimeamua kuwasamehe wafungwa 61 waliokuwa wamehukumiwa kunyongwa. Lakini katika kuchunguzwa kwingi wapo wafungwa ambao wametubu dhambi zao, wamekiri makosa yao kwelikweli,” alisema Magufuli.
Mwaka 2003, Babu Seya na wanaye watatu walikamatwa na kufunguliwa mashtaka ya kubaka na kulawiti watoto wa Shule ya Msingi Mashujaa, mwaka 2004, Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar iliwahukumu wote wanne kifungo cha maisha jela.
Baada ya hukumu hiyo, walikata rufaa lakini mwaka 2005, Mahakama Kuu iliridhia hukumu hiyo ya kifungo cha maisha jela kwa wote wanne kabla ya Mahakama ya Rufaa kuwaachia huru Mbangu na Chichi Februari 2010.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu