Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Harley ameapa kuyataja mataifa yanaounga mkono Korea Kaskazini na mpango wake wa kinyuklia huku hali ya wasiwasi ikiendelea.

In Kimataifa

Balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa Nikki Harley ameapa kuyataja mataifa yanaounga mkono Korea Kaskazini na mpango wake wa kinyuklia huku hali ya wasiwasi ikiendelea.

Matamshi yake yanajiri kufuatia mkutano wa dharura wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa.

Baraza hilo siku ya Jumatatu kwa pamoja lilishutumu jaribio la kombora la masafa marefu lililotekelezwa na Korea Kaskazini na kuonya kuhusu vikwazo vipya.

Korea kaskazini inesema kuwa kombora hilo lililofanyiwa majaribio ni jipya na lina uwezo wa kubeba kichwa cha kinyuklia.

Lilisafiri urefu wa kilomita 700 na kwenda juu kilomita 2000 kabla ya kuanguka magharibi mwa bahari ya Japan.

Hatahivyo Korea Kusini ilishindwa kubaini habari hiyo.

Akizungumza katika mkutano wa faragha wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa siku ya Jumanne , bi Harley aliyaonya mataifa yanayounga mkono Korea Kaskazini kuwacha kauli hiyo la sivyo yaone cha mtema kuni.

Washington alisema, inaunga mkono mazungumzo na Pyongyang iwapo taifa hilo litasitisha majaribio ya makombora ya masafa marefu na yale ya kinyuklia

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu