Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limewataka Waislamu kujiepusha na mtu anayejiita mtume

In Kitaifa

Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata) limewataka Waislamu kujiepusha na mtu anayejiita mtume na kufundisha mambo yanayopingana na Imani ya Kiislamu, eneo la Kibaha Misugusugu mkoani Pwani.

Akizungumza kwa niaba ya Mufti Shehe Mkuu wa Tanzania, Abubakar Zubeir jijini Dar es Salaam jana, Msemaji wa Mufti, Shehe Khamis Mataka  amesema Hamza Issa ndiye anayedai kushukiwa na roho ya Nabii Illyasa na kuwaaminisha watu kwenye mafundisho yake kuwa yeye ndiye Nabii Ilyasa.

Amesema baada ya kupokea maazimio ya Baraza la Mashehe wa Mkoa wa Pwani kuhusu taarifa za Hamza Issa kujiita mtume, Mufti Zubeir alikaa na Baraza lake la Ulamaa na kupitisha maazimio mbalimbali ikiwemo kuwaonya Waislamu, kuwa yeyote atakayemfuata Hamza Issa, atakuwa ametoka ndani ya Uislamu.

Shehe Mataka alitaja maazimio mengine yaliyopitishwa na Baraza la Ulamaa ni pamoja na kuwataka mashehe wa mikoa, wilaya na Maimamu, kutompa nafasi Hamza Issa ya kuzungumza misikitini wala kusikiliza CD zake ,ili kutoruhusu upotoshaji wake kuenea katika jamii.

Msemaji huyo wa Mufti alieleza kuwa Baraza la Ulamaa ni chombo cha kuchunga nidhamu ya dini katika Uislamu na kuongeza kuwa mafundisho yanayotolewa na Hamza Issa, kuhusu kuingiwa na roho ilyomfanya kuwa mtume ni mara ya kwanza kusikika duniani kwa mujibu wa Imani ya Kiislamu.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu