Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta) limewataka watumishi wote wenye malalamiko kuhusu uhakiki wa vyeti vyao kupeleka malalamiko yao kwa Katibu Mkuu ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

In Kitaifa

SIKU chache baada ya kuwekwa hadharani majina ya watumishi walioghushi vyeti na wenye malalamiko kuanza kumiminika katika ofisi za Baraza la Mitihani la Tanzania (Necta), kutaka ufafanuzi wa uhakiki wa taarifa zao, baraza hilo limewataka watumishi hao kupeleka kwa maandishi malalamiko yao kwa Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma.

Pamoja na Necta kuwataka watumishi hao kwenda kwa Katibu Mkuu Ofisi ya Rais-Menejimenti ya Utumishi wa Umma, walipofika katika ofisi hizo, malalamiko yao hayakupokelewa, kwa kile walichoelezwa kuwa NECTA inapaswa kuwapa taarifa ya nini cha kufanya na hawakuwa na taarifa hiyo bado mpaka jana.

Hata hivyo wakati hayo yakijiri, Waziri katika Ofisi ya Rais, Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Angella Kairuki, alipoulizwa kuhusu suala hilo, alilieleza gazeti hili mjini Dodoma jana kuwa Katibu Mkuu wa Ofisi hiyo, atalitolea ufafanuzi leo mjini humo.

Hivi karibuni Rais, John Magufuli alikabidhiwa taarifa ya uhakiki wa vyeti kwa watumishi wa umma ambapo watumishi zaidi ya 9,932 walibainika kuwa na vyeti vya kughushi na alitangaza kuwafuta kazi na aliwapa siku 15, wawe wameondoka kazini, la sivyo watachukuliwa hatua za kisheria.

Katibu Mkuu Ofisi ya Rais -Menejimenti ya Utumishi wa Umma, alichapisha sehemu ya kwanza majina ya watumishi hao katika vyombo vya habari na jana baadhi ya watumishi walianza kumiminika katika ofisi za Necta, kutaka kujua kasoro za vyeti vyao.

Katika kushughulikia tatizo hilo, Baraza hilo kupitia kwa Katibu Mtendaji wake, Dk Charles Msonde limewataka watumishi wa umma wenye malalamiko kuhusu matokeo ya uhakiki wa vyeti vyao, wawasilishe malalamiko yao kwa maandishi kwa Katibu Mkuu Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora kupitia kwa waajiri wao na barua hizo za malalamiko, ziambatanishwe na nakala za vyeti husika.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu