Baraza la Seneti lapitisha Mswada wa kuwawekea vikwazo Urusi, iran na korea Kaskazini

In Kimataifa

Baraza la Seneti la Marekani kwa sauti moja hapo jana limepitisha mswada wa kuziwekea vikwazo vipya Urusi, Iran na Korea Kaskazini, na kuuwasilisha mswada huo kwa Rais Donald Trump ambaye sasa anatakiwa kufanya uamuzi wa kutia saini ili ugeuke kuwa sheria.

Mswada huo unamzuia rais Trump kuipunguzia vikwazo Urusi bila ya idhini ya seneti.

Trump amekuwa akisisitiza mara kwa mara juu ya kuwepo kwa uhusiano mzuri na Urusi, licha ya uchunguzi uliofanywa mara kadhaa kuhusu Urusi kuingilia uchaguzi wa rais wa mwaka jana uliomuweka Trump madarakani.

Vikwazo dhidi ya Korea ya Kaskazini vinalenga silaha zake za nyuklia na mpango wake wa makombora na Iran inalengwa kwa shughuli zake za kigaidi, ukiukwaji wa haki za binadamu pamoja na mipango ya makombora ya masafa marefu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu