Baraza la Seneti lapitisha Mswada wa kuwawekea vikwazo Urusi, iran na korea Kaskazini

In Kimataifa

Baraza la Seneti la Marekani kwa sauti moja hapo jana limepitisha mswada wa kuziwekea vikwazo vipya Urusi, Iran na Korea Kaskazini, na kuuwasilisha mswada huo kwa Rais Donald Trump ambaye sasa anatakiwa kufanya uamuzi wa kutia saini ili ugeuke kuwa sheria.

Mswada huo unamzuia rais Trump kuipunguzia vikwazo Urusi bila ya idhini ya seneti.

Trump amekuwa akisisitiza mara kwa mara juu ya kuwepo kwa uhusiano mzuri na Urusi, licha ya uchunguzi uliofanywa mara kadhaa kuhusu Urusi kuingilia uchaguzi wa rais wa mwaka jana uliomuweka Trump madarakani.

Vikwazo dhidi ya Korea ya Kaskazini vinalenga silaha zake za nyuklia na mpango wake wa makombora na Iran inalengwa kwa shughuli zake za kigaidi, ukiukwaji wa haki za binadamu pamoja na mipango ya makombora ya masafa marefu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu