Bodi 10 za vyama vya ushirika zavunjwa wilayani Nachingwea Mkoani Lindi.

In Kitaifa

SERIKALI kupitia Maraisi wa Vyama vya Ushirika imeanza kuchukua hatua dhidi ya ubadhirifu wa fedha na mali za vyama hivyo nchini ,baada ya kuvunja bodi 10 za vyama hivyo vya wakulima wa korosho wilayani Nachingwea mkoani Lindi.

Aidha, makatibu wakuu 10 wa vyama hivyo wameondolewa madarakani, na bodi mpya za muda zimewekwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika.

Kaimu Mrajisi Msaidizi, Revocatus Nyagilo ambaye ameongoza vikao vya kuvunjwa bodi hizo kwa niaba ya mrajisi wilayani Nachingwea, amesema hatua hiyo inatokana na uchunguzi uliofanywa na Serikali kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini (TCDC), kwa kushirikiana na Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO).

Nyagilo amesema uchunguzi huo uliofanyika mwaka jana, ulibaini ubadhirifu wa mabilioni ya fedha na mali, katika vyama hivyo katika mikoa ya Lindi na Mtwara na hivyo kuamua kuitisha mikutano maalum ya vyama hivyo, katika mikoa hiyo kwa hatua zaidi.

Katika taarifa fupi ya utekelezaji wa kazi hiyo wilayani Nachingwe imeeleza kuwa ,vyama ambavyo bodi zake zimeondolewa madarakani na makatibu kuvuliwa nafasi zao Aprili 20 mwaka huu kwa ubadhirifu ni Ndomondo, Naipanga, Chiumbati, New Stesheni na Mchonda.

Vingine ni Makina, Mkotokuyana, Nache, Namikango na Ndanga limbo,Vyote 10 ni Vyama vya Ushirika vya Mazao na Masoko (AMCOS) na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote waliohusika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu