Bodi 10 za vyama vya ushirika zavunjwa wilayani Nachingwea Mkoani Lindi.

In Kitaifa

SERIKALI kupitia Maraisi wa Vyama vya Ushirika imeanza kuchukua hatua dhidi ya ubadhirifu wa fedha na mali za vyama hivyo nchini ,baada ya kuvunja bodi 10 za vyama hivyo vya wakulima wa korosho wilayani Nachingwea mkoani Lindi.

Aidha, makatibu wakuu 10 wa vyama hivyo wameondolewa madarakani, na bodi mpya za muda zimewekwa kwa mujibu wa Sheria ya Vyama vya Ushirika.

Kaimu Mrajisi Msaidizi, Revocatus Nyagilo ambaye ameongoza vikao vya kuvunjwa bodi hizo kwa niaba ya mrajisi wilayani Nachingwea, amesema hatua hiyo inatokana na uchunguzi uliofanywa na Serikali kupitia Tume ya Maendeleo ya Ushirika nchini (TCDC), kwa kushirikiana na Shirika la Ukaguzi na Usimamizi wa Vyama vya Ushirika (COASCO).

Nyagilo amesema uchunguzi huo uliofanyika mwaka jana, ulibaini ubadhirifu wa mabilioni ya fedha na mali, katika vyama hivyo katika mikoa ya Lindi na Mtwara na hivyo kuamua kuitisha mikutano maalum ya vyama hivyo, katika mikoa hiyo kwa hatua zaidi.

Katika taarifa fupi ya utekelezaji wa kazi hiyo wilayani Nachingwe imeeleza kuwa ,vyama ambavyo bodi zake zimeondolewa madarakani na makatibu kuvuliwa nafasi zao Aprili 20 mwaka huu kwa ubadhirifu ni Ndomondo, Naipanga, Chiumbati, New Stesheni na Mchonda.

Vingine ni Makina, Mkotokuyana, Nache, Namikango na Ndanga limbo,Vyote 10 ni Vyama vya Ushirika vya Mazao na Masoko (AMCOS) na hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya wote waliohusika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu