Bodi ya korosho Tanzania yaongeza vituo vya ugawaji pembejeo.

In Kitaifa

Bodi ya korosho Tanzania imeongeza vituo vya ugawaji pembejeo ili kuharakisha usambazaji na kuhakikisha kila mkulima anapata pembejeo kwa wakati katika kudhibiti kuenea kwa magonjwa na wadudu wanaoshambulia zao la korosho.

Akitolea ufafanuzi tuhuma za ucheleweshwaji wa madawa na viuatilifu Mwanasheria na Katibu wa Bodi hiyo, Ugumba Kilasa amesema kuwa bado wapo ndani ya wakati kwa kuwa matumizi ya viuatilifu huanza mara tu korosho zinapotoa maua mwezi Juni.

Amesema kuwa kufikia Agosti 20, 2017 usambazaji wa pembejeo kwa wakulima wote kwa msimu mpya utakuwa umekamilika kwani tani zilizobaki kukamilisha usambazaji kwa wakulima wote tayari zimeingia bandarini na zipo katika taratibu za kutolewa ili kusambazwa.

Hata hivyo,  amewaonya wale wanaotoa maneno ya kuwavunja moyo wakulima wa zao hilo kuhusu kusambazwa kwa madawa na viuatilifu kwambi si huduma ya bure na kusema kwamba serikali imeamua kutoa madawa hayo kwa wakulima bure na kila mtu atapata kulingana na mgawo wa madawa hayo

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu