BOMU LAUWA WATANO SOMALIA

In Kimataifa

Polisi pamoja na mashuhuda nchini  Somalia wamesema kwamba bomu lenye nguvu la kwenye gari Jumapili limeua takriban watu watano nje ya mgahawa maarufu katikati mwa nchi. 

Wanamgambo wenye uhusiano na kundi la kigaidi la al Qaida wamedai kuhusika na sh,ambulizi hilo. Mlipuko huo pia umewajeruhi watu wengine 14 pamoja na kuharibu majengo mengine karibu na mgahawa huo kwenye mji wa Jowhar ulioko takriban kilomita 90 kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, washambuliaji waliendesha gari lililojaa vilipuzi kwenye ukuta wa mgahawa wa Nur-doop, ambao ni maarufu sana miongoni mwa wabunge pamoja na maafisa wa serikali. Afisa wa usalama Mohamed Ali kutoka mjini humo alisema kwamba miongoni mwa watu waliokufa ni wanawake waliokuwa wakifanya kazi kwenye mgahawa huo.

Waziri mkuu mpya Hamza Abdi Barre aliyeidhinishwa na bunge mwezi Juni ametuma salaam za rambi rambi kwa waathirika huku akiahidi msaada wa serikali kwa wale waliojeruhiwa kwenye mkasa huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu