BOMU LAUWA WATANO SOMALIA

In Kimataifa

Polisi pamoja na mashuhuda nchini  Somalia wamesema kwamba bomu lenye nguvu la kwenye gari Jumapili limeua takriban watu watano nje ya mgahawa maarufu katikati mwa nchi. 

Wanamgambo wenye uhusiano na kundi la kigaidi la al Qaida wamedai kuhusika na sh,ambulizi hilo. Mlipuko huo pia umewajeruhi watu wengine 14 pamoja na kuharibu majengo mengine karibu na mgahawa huo kwenye mji wa Jowhar ulioko takriban kilomita 90 kaskazini mwa mji mkuu wa Mogadishu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP, washambuliaji waliendesha gari lililojaa vilipuzi kwenye ukuta wa mgahawa wa Nur-doop, ambao ni maarufu sana miongoni mwa wabunge pamoja na maafisa wa serikali. Afisa wa usalama Mohamed Ali kutoka mjini humo alisema kwamba miongoni mwa watu waliokufa ni wanawake waliokuwa wakifanya kazi kwenye mgahawa huo.

Waziri mkuu mpya Hamza Abdi Barre aliyeidhinishwa na bunge mwezi Juni ametuma salaam za rambi rambi kwa waathirika huku akiahidi msaada wa serikali kwa wale waliojeruhiwa kwenye mkasa huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu