Bunge limepitisha sheria mpya ambayo sasa itatambua haki na dhamana ya serikali katika makinikia

In Kitaifa

Bunge limepitisha sheria mpya ambayo sasa itatambua haki na dhamana ya serikali katika makinikia, ambayo itakuwa ni marufuku kuchenjuliwa nje ya nchi.

Sheria hiyo inaeleza kuwa serikali itashiriki kwa asilimia kuanzia 16 hadi 50 katika shughuli zote za uchimbaji, uchakataji na uchejuaji madini, na ununuzi wa hisa katika kampuni ya uchimbaji madini.

Aidha Wakala wa Ukaguzi wa Madini TMAA umefutwa rasmi, na sasa kunaanzishwa Kamisheni ya Madini.

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi amesema kufutwa kwa TMAA, kunatokana na majukumu yake yaliyokuwa yakitekelezwa na wakala huyo, kuhamishiwa kwa Kamisheni ya Madini.

Kuanzia sasa umiliki wa leseni mbalimbali zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Madini,hautahamishwa kabla haujafanyiwa uendelezaji katika kitalu husika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu