Bunge limepitisha sheria mpya ambayo sasa itatambua haki na dhamana ya serikali katika makinikia

In Kitaifa

Bunge limepitisha sheria mpya ambayo sasa itatambua haki na dhamana ya serikali katika makinikia, ambayo itakuwa ni marufuku kuchenjuliwa nje ya nchi.

Sheria hiyo inaeleza kuwa serikali itashiriki kwa asilimia kuanzia 16 hadi 50 katika shughuli zote za uchimbaji, uchakataji na uchejuaji madini, na ununuzi wa hisa katika kampuni ya uchimbaji madini.

Aidha Wakala wa Ukaguzi wa Madini TMAA umefutwa rasmi, na sasa kunaanzishwa Kamisheni ya Madini.

Waziri wa Katiba na Sheria Profesa Palamagamba Kabudi amesema kufutwa kwa TMAA, kunatokana na majukumu yake yaliyokuwa yakitekelezwa na wakala huyo, kuhamishiwa kwa Kamisheni ya Madini.

Kuanzia sasa umiliki wa leseni mbalimbali zinazotolewa kwa mujibu wa Sheria ya Madini,hautahamishwa kabla haujafanyiwa uendelezaji katika kitalu husika.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu