Cairo jiji hatari zaidi kwa wanawake duniani.

In Kimataifa

Jiji la Cairo ndilo hatari zaidi kwa wanawake kuishi duniani miongoni mwa majiji duniani, utafiti wa shirika la Thomson Reuters Foundation unaonesha.
London nao ndio mji bora zaidi kwa wanawake kuishi.
Mji wa Kishasha nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo unafuata Cairo, nao mji wa Lagos nchini Nigeria ni wa nane kwenye orodha hiyo.
Jumla ya majiji 19 makubwa yalichunguzwa – ambayo ni majiji yenye idadi ya watu inayofika milioni kumi na zaidi.
Miongoni mwa yaliyozingatiwa kwenye utafiti huo ni unyanyasaji wa kingono, utamaduni unaowadhalilisha wanawake pamoja na upatikanaji wa huduma bora ya afya kwa wanawake, fedha na elimu.
Wataalamu katika haki za wanawake waliombwa ushauri wao wakati wa kufanywa kwa utafiti hao, miongoni mwao akiwa mwanahabari Shahira Amin, ambaye aliambia Thomson Reuters:
“Mambo yote kuhusu wanawake katika jiji hilo ni hatari. Hata kutembea tu barabarani, na hunyanyaswa sana, kwa maneno na kwa vitendo.”

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu