Cannavaro aongoza mazungumzo na wachezaji kuhusiana na mgomo wao.

In Kitaifa, Michezo

Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro’ amezungumza na wachezaji wenzake kuhusiana na suala lao la kugoma.
Cannavaro, amezungumza na wachezaji wenzake kwenye Uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, muda mchache kabla ya kuanza mazoezi.
Wakati akizungumza na wachezaji hao, tayari benchi la ufundi likiongozwa na Kocha George Lwandamina lilikuwa limeanza kufanya mazungumzo na wachezaji hao ambao jana waligoma kufanya mazoezi wakitaka kulipwa mishahara yao ya miezi miwili.
Baada ya mazungumzo hayo yaliyoanza takribani saa 3:30 asubuhi, hatimaye wachezaji wa Yanga walirejea kazini na kuanza mazoezi saa 3:47.

 

Walifanya mazoezi kwa takribani saa moja ana ushee na taarifa zinaeleza kuwa wameahidiwa suala lao kushughulikiwa.
Hivi karibuni, Cannavaro alikutana na Mwenyekiti wa zamani wa Yanga, Yusuf Manji aliyekuwa katika mahakama ya Kisutu na kuzungumza naye kwa muda, kitendo kilichozua gumzo

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu