Chadema wajitoa uchaguzi mdogo Arumeru.

In Kitaifa, Siasa

Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe ametangaza kujitoa katika uchaguzi mdogo unaondelea kufanyika katika jimbo LA arumeru mashariki kwa madai kuwa uchaguzi huo sio huru na wa haki.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini arusha mbowe amesema kuwa kutokana na dosari zilizojitokeza anaagiza kuanzia sasa mawakala,wagombea na viongozi wa chama kuondoka katika vituo vya uchaguzi.

Aidha amesema kuwa sababu zilizopeleka kujiondoa ni kutokana na mawakala kushindwa kuongia katika vituo vya kura asubuhi kwa madai ya kukosa fomu ya utambulisho ambayo hutolewa na msimamizi mkuu wa uchaguzi.

Ameendelea kusema kuwa wanaitaka tume ya uchaguzi kufanya uchunguzi wa kina kwa kuwa yapo matukio mengi yamejitokeza ya ikiwemo kujeruhiwa kwa watu,mawakala na vipo vituo ambavyo mawakala hawajaingia kabisa.

Nao baadhi ya wagombea akiwepo mgombea wa kata ya Makiba Joyce Martin amesema katika kata yake wananchi wamejeruhiwa vibaya.

Kata hizo ni Maroroni, Makiba,Ambureni, Ngabobo na Leguruki ambapo bado uchaguzi unaendelea kwa sasa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu