Chadema wajitoa uchaguzi mdogo Arumeru.

In Kitaifa, Siasa

Mwenyekiti wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA Freeman Mbowe ametangaza kujitoa katika uchaguzi mdogo unaondelea kufanyika katika jimbo LA arumeru mashariki kwa madai kuwa uchaguzi huo sio huru na wa haki.

Akizungumza na vyombo vya habari jijini arusha mbowe amesema kuwa kutokana na dosari zilizojitokeza anaagiza kuanzia sasa mawakala,wagombea na viongozi wa chama kuondoka katika vituo vya uchaguzi.

Aidha amesema kuwa sababu zilizopeleka kujiondoa ni kutokana na mawakala kushindwa kuongia katika vituo vya kura asubuhi kwa madai ya kukosa fomu ya utambulisho ambayo hutolewa na msimamizi mkuu wa uchaguzi.

Ameendelea kusema kuwa wanaitaka tume ya uchaguzi kufanya uchunguzi wa kina kwa kuwa yapo matukio mengi yamejitokeza ya ikiwemo kujeruhiwa kwa watu,mawakala na vipo vituo ambavyo mawakala hawajaingia kabisa.

Nao baadhi ya wagombea akiwepo mgombea wa kata ya Makiba Joyce Martin amesema katika kata yake wananchi wamejeruhiwa vibaya.

Kata hizo ni Maroroni, Makiba,Ambureni, Ngabobo na Leguruki ambapo bado uchaguzi unaendelea kwa sasa.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu