Chadema yatoa taarifa juu ya Mbowe kushambuliwa

In Kitaifa


Usiku wa kuamkia leo kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani
Bungeni ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chama Cha Chadema
Freeman Aikael Mbowe, amevamiwa nyumbani kwake jijini
Dodoma na watu wasiojulikana ambao walimpiga na kumjeruhi.
Katibu Mkuu wa Chadema John Mnyika amesema waliomvamia
Mbowe bado hawajajulikana,lakini wakati wa tukio walisema
maneno yenye muelekeo wa kisiasa.
Kwa sasa Mbowe amehamishiwa jijini Dar es Salaam kwa ajili
ya matibabu zaidi.

Kufutia tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma Gilles
Muroto amesema jeshi hilo linaendelea na uchunguzi lakini kwa
taarifa za awali, Mbowe ameumizwa kwa kukanyagwa na
kuvunjika mguu wa kulia.

Rais Dkt John Magufuli pia amefika kumjulia hali Mwenyekiti
wa CHADEMA Taifa na Kiongozi wa Kambi Rasmi ya

Upinzani Bungeni Freeman Mbowe ambaye ameshambuliwa na
kujeruhiwa na watu wasiojulikana wakati akirejea nyumbani
kwake Area D jijijini Dodoma usiku wa kuamkia leo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu