Chama cha ACT-Wazalendo kimemvua uenyekiti wa chama hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kufuatia uteuzi wake.

In Kitaifa

Chama cha ACT-Wazalendo kimemvua uenyekiti wa chama hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kufuatia uteuzi wake.

Uamuzi huo umetangazwa leo na Katibu Mkuu wa chama hicho, Samsoni Mwigamba alipofanya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mwigamba alisema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kubaini kuwa kutokana na uteuzi huo, Mghwira hawezi kufanya kazi ya uenyekiti wa chama hicho kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo wa chama amesifia uamuzi wa Rais John Magufuli kuwateua watu kutoka upande wa upinzani, lakini ameomba kamati ya uongozi kumshauri kuweka mfumo bora wa kufanya uteuzi kutoka upande wa upinzani ili kuepusha migongano.

Mama Mghwira aligombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika uchaguzi mkuu uliopita kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu