Chama cha ACT-Wazalendo kimemvua uenyekiti wa chama hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kufuatia uteuzi wake.

In Kitaifa

Chama cha ACT-Wazalendo kimemvua uenyekiti wa chama hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kufuatia uteuzi wake.

Uamuzi huo umetangazwa leo na Katibu Mkuu wa chama hicho, Samsoni Mwigamba alipofanya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mwigamba alisema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kubaini kuwa kutokana na uteuzi huo, Mghwira hawezi kufanya kazi ya uenyekiti wa chama hicho kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo wa chama amesifia uamuzi wa Rais John Magufuli kuwateua watu kutoka upande wa upinzani, lakini ameomba kamati ya uongozi kumshauri kuweka mfumo bora wa kufanya uteuzi kutoka upande wa upinzani ili kuepusha migongano.

Mama Mghwira aligombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika uchaguzi mkuu uliopita kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu