Chama cha ACT-Wazalendo kimemvua uenyekiti wa chama hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kufuatia uteuzi wake.

In Kitaifa

Chama cha ACT-Wazalendo kimemvua uenyekiti wa chama hicho, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira kufuatia uteuzi wake.

Uamuzi huo umetangazwa leo na Katibu Mkuu wa chama hicho, Samsoni Mwigamba alipofanya mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Mwigamba alisema kuwa uamuzi huo umefikiwa baada ya kubaini kuwa kutokana na uteuzi huo, Mghwira hawezi kufanya kazi ya uenyekiti wa chama hicho kwa ufanisi.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo wa chama amesifia uamuzi wa Rais John Magufuli kuwateua watu kutoka upande wa upinzani, lakini ameomba kamati ya uongozi kumshauri kuweka mfumo bora wa kufanya uteuzi kutoka upande wa upinzani ili kuepusha migongano.

Mama Mghwira aligombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, katika uchaguzi mkuu uliopita kwa tiketi ya chama cha ACT-Wazalendo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu