Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kanda ya kati kimeitaka serikali kuwalipa fidia wakazi wa Manispaa ya Dodoma ambao kwa namna moja au nyingine wameathirika na vitendo vya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kuwapora ardhi yao.

In Kitaifa

Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kanda ya kati kimeitaka serikali kuwalipa fidia wakazi wa Manispaa ya Dodoma ambao kwa namna moja au nyingine wameathirika na vitendo vya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kuwapora ardhi yao.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Mafunzo na oganaizesheni wa Chadema, BENSON KIGAILA wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Dodoma.
Amesema kuwa Rais hawezi kuivunja CDA na ikawa ndiyo mwisho wake bila kuangalia madhara yaliyosababishwa na mamlaka hiyo ,kwa wananchi katika kipindi chote cha miaka 44 iliyofanya kazi.
Mbali na hilo aliwapongeza wakazi wa Manispaa ya Dodoma pamoja na viongozi wao, kwa kupaza sauti kwa nguvu dhidi ya uonevu uliokuwa unafanywa na CDA na hatimaye kupelekea Rais kuivunja rasmi.

CDA ilianzishwa kwa amri ya Rais, Aprili mosi, mwaka 1973 na kutangazwa kupitia tangazo la Serikali namba 230 na kuvunjwa Mei 15, 2017 kwa Amri ya Rais na kuchapishwa katika gazeti la Serikali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu