Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kanda ya kati kimeitaka serikali kuwalipa fidia wakazi wa Manispaa ya Dodoma ambao kwa namna moja au nyingine wameathirika na vitendo vya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kuwapora ardhi yao.

In Kitaifa

Chama cha demokrasia na maendeleo (Chadema) kanda ya kati kimeitaka serikali kuwalipa fidia wakazi wa Manispaa ya Dodoma ambao kwa namna moja au nyingine wameathirika na vitendo vya Mamlaka ya Ustawishaji Makao Makuu (CDA) kwa kuwapora ardhi yao.

Kauli hiyo imetolewa leo na Mkurugenzi wa Mafunzo na oganaizesheni wa Chadema, BENSON KIGAILA wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake mjini Dodoma.
Amesema kuwa Rais hawezi kuivunja CDA na ikawa ndiyo mwisho wake bila kuangalia madhara yaliyosababishwa na mamlaka hiyo ,kwa wananchi katika kipindi chote cha miaka 44 iliyofanya kazi.
Mbali na hilo aliwapongeza wakazi wa Manispaa ya Dodoma pamoja na viongozi wao, kwa kupaza sauti kwa nguvu dhidi ya uonevu uliokuwa unafanywa na CDA na hatimaye kupelekea Rais kuivunja rasmi.

CDA ilianzishwa kwa amri ya Rais, Aprili mosi, mwaka 1973 na kutangazwa kupitia tangazo la Serikali namba 230 na kuvunjwa Mei 15, 2017 kwa Amri ya Rais na kuchapishwa katika gazeti la Serikali.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Serikali kuunga mkono juhudi za Taasisi mbali mbali.

Rais wa Zanzibar Dkt Hussein Mwinyi, amesema serikaliitaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Taasisi yaZanzibar Maisha Bora Foundation,pamoja na

Read More...

DKT. KIRUSWA AZINDUA MFUMO WA USHIRIKISHWAJI WA WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI

Watanzania waendelea kunufaika Sekta ya Madini, ajira 15,341 zamwagwa, manunuzi ya ndani ya nchi yafikia Dola za Marekani bilioni

Read More...

MAFURIKO YAUWA 190 MALAWI

Takriban watu 190 sasa wamethibitishwa kufariki nchini Malawi baada ya Dhoruba ya Mafuriko ya Tropiki Freddy kulikumba eneo

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu