Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea kwa mshutuko mkubwa kifo cha Muasisi wa chama hicho na mbunge wa mstaafu wa jimbo la Moshi PHILIMON NDESAMBURO mwenye umri wa miaka(84).

In Kitaifa

Chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimepokea  kwa mshutuko mkubwa kifo cha Muasisi wa chama hicho na mbunge wa mstaafu wa jimbo la Moshi PHILIMON NDESAMBURO mwenye umri wa miaka(84).

NDESAMBURO ambaye alikuwa mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini kwa mfululizo wa miaka 15, na aliamua kustaafu kwa heshima huku akiendelea kuimarisha chama pamoja akiwa na nafasi ,ya kuwa mwenyekiti wa kanda katika mkoa wa Kilimanjaro.

Mauti yamemkuta mwasisi wa chama hicho akiwa katika maadalizi ya kuandika cheki ya kiasi cha sh. Milioni 3.5 ,kama sehemu ya rambirambi kwa ajili ya wanafunzi 35 waliopata ajali na kupoteza maisha katika shule ya msingi ya Lacky Vicent.

Akizungumza na waandishi wa habari katika ukumbi wa mikutano wa Bunge, Mwenyekiti wa Chadema Taifa,FREEMAN MBOWE amesema kifo cha Mwasisi huyo ni msiba mkubwa kwa wanachadema na wakazi wa Mji wa Moshi kwa ujumla kutokana na jinsi alivyoweza kujenga ushirikino na umoja wakati wa utawala uongozi wake.

 MBOWE  amesema mwasisi huyo alikuwa katika vikao wa baraza kuu la Chadema, vilivyofanyikia mjini Dodoma aliweza kurejea moshi akiwa na nguvu zake bila kuwa na viashiria vyovyote vya ugonjwa.

Hata hivyo amesema mwasisi huyo baada ya kumaliza vikao vya baraza kuu la Chadema, alirudi moshi na jana  alimpigia simu meya wa Jiji la Arusha KALIST LAZARO, ili afike nyumbani kwake moshi kwa ajili ya kumpatia rambirambi kwa ajili ya watoto ambao walipata ajali na kupoteza maisha katika shule ya msingi Luckly Vicent.

Amesema wakati wa maongezi hayo alitaka kujua waathirika wa ajari hiyo walikuwa wangapi na ndipo Meya alipomweleza kuwa walikuwa 35, ambapo alikuwa amekubali kutoa kiasi cha sh.laki moja kwa kila mwathirika kiasi cha jumla y ash. Milioni 3.5.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu