CHAMA cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa) kimesisitiza kuwa kuwafukuza wasichana wanaopata mimba shuleni ni kunyima haki yao ya kupata elimu.

In Kitaifa

CHAMA cha Wanahabari Wanawake Tanzania (Tamwa) kimesisitiza kuwa kuwafukuza wasichana wanaopata mimba shuleni ni kunyima haki yao ya kupata elimu.

Kimesema hatua hiyo ni sawa na kuwafungia milango ya maendeleo wakati elimu ndio njia ya kuwatoa katika umaskini.

Tamwa imesema hayo baada ya wabunge, hususan wabunge wanawake kutaka wasichana kufukuzwa shule, pindi wanapopewa mimba kukomesha tatizo hilo.

Wabunge walitoa msimamo huo wakati wa kujadili hotuba ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako katika kikao cha Bunge kinachoendelea mjini Dodoma.

Taarifa ya Tamwa iliyotolewa kwa vyombo vya habari jana ilieleza mazingira ya shule wanakosoma wasichana hao siyo rafiki kwa wanafunzi wa kike na makundi rika ambayo husababisha watoto pia kufundishana na kushiriki katika matendo ya ngono zembe. Ilisema matokeo ya matendo hayo ni mimba, Ukimwi na magonjwa ya zinaa.

Tamwa imesema dhana kuwa wanaopata mimba shuleni wasiruhusiwe kuendelea kwa kuwa wamejifukuzisha na ya kuwaruhusu kuendelea na shule wakijifungua ni kuongeza mimba mashuleni haina ukweli.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu