Chama cha watu wenye ualbino nchini(TASI),kimeitaka serikali kuhakikisha inafuatalia kwa ukaribu matukio mbalimbali ambayo wanakutananayo kwa kuyapa uzito kama ilivyo kuwa kwa Faru John.

In Kitaifa

Chama cha watu wenye ualbino nchini(TASI),kimeitaka serikali kuhakikisha inafuatalia kwa ukaribu matukio mbalimbali ambayo wanakutananayo kwa kuyapa uzito kama ilivyo kuwa kwa Faru John.

Kauli hiyo imetolewa leo Mjini Dodoma na Mwenyekiti wa Chama hicho Taifa,Colman Temba wakati wa mkutano na waandishi wa habari  ambapo amesema licha ya serikali kuonyesha juhudi za kupambana na ukatili kwa watu wenye ualbino lakini bado kuna mapungufu makubwa.

Aidha amebainisha kuwa   licha ya Serikali kupitisha sheria ya makosa ya mtandao bado sheria hizo zimekuwa zikiwalenga watu ambao wanaonekana kuwa na nafasi kubwa serikalini lakini siyo katika jamii ya watu wenye ualbino.

Katika hatua nyingine Waziri wa Nchi,Ofisi ya Waziri Mkuu,sera Bunge,Ajira,Vijana na Watu wenye Ulemavu,JENISTER MHAGAMA anatarajiwa kuwa ngeni rasmi katika Maadhimisho ya siku ya Kimataifa ya uelewa juu ya watu wenye ualbino mjini Dodoma.

TEMBA amesema maadhimisho hayo yanalenga Takwimu na Tafiti kwa ustawi wa kutoa elimu kwa jamii ili kuhakikisha wanatambua umuhimu wa kuwepo ikiwa ni pamoja na  kushirikiana na watu wenye ulemavu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu