Chama kinachoongozwa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kimeibuka na ushindi wa viti vingi katika bunge la nchi hiyo, wiki kadhaa baada ya ushindi wake wa nafasi hiyo ya Urais.

In Kimataifa
Chama kinachoongozwa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kimeibuka na ushindi wa viti vingi katika bunge la nchi hiyo, wiki kadhaa baada ya ushindi wake wa nafasi hiyo ya Urais.
Zikiwa karibu kura zote zimehesabiwa chama chake cha Republique en Merche, sambamba na washirika wao MoDem, walipata zaidi ya viti 300 kati ya viti 577 vya bunge la nchi hiyo.
Akilihutubia taifa Waziri mkuu wa Ufaransa, Edouard Phillippe, amesema amezielezea kura hizo zilizopigwa kuwa ni za matumaini.
Chama hicho kinachoongozwa na Rais Macron kiliundwa tu mwaka uliopita na nusu ya wagombea wake wana udhoefu mdogo wa masuala ya kisiasa huku wengine wakiwa hawana kabisa.
Matokeo hayo ya kura yamempa nguvu na uwezo Rais huyo mwenye umri wa miaka 39 wa kuwa na mamlaka ndani ya bunge la nchi hiyo na kuweza kuendelea na msimamo wake wa kufanya mabadiliko aliyoyanadi katika kampeni zake za uchaguzi.
Lakini hata hivyo, wapiga kura wachache walijitokeza katika awamu hiyo ya pili ya uchaguzi wa Bunge, kushinda ilivyo tarajiwa, huku rekodi yake ikikadiriwa kushuka kwa karibu asilimia 42, kulinganisha na miaka mitano iliyopita.
Katika uchaguzi huo, kiuongozi wa chama cha mrengo wa kulia Marine Le Pen, alipata ushindi kwa mara ya kwanza.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu