Chama tawala cha Rwanda Patriotic Front RPF kimetangaza kuanza kampeni za urais ijumaa katika mkoa wa Kusini.

Chama tawala cha Rwanda Patriotic Front RPF kimetangaza kuanza kampeni za urais ijumaa katika mkoa wa Kusini.

Mwezi uliopita Chama cha RPF kilimchagua rais wa sasa Paul Kagame wa Rwanda kuwa mgombea urais wa chama hicho, atakayeshindana na Frank Habineza wa chama cha kijani, na mgombea huru Philipe Mpayimana.

Katibu mkuu wa chama cha RPF Bw Francois Ngarambe amesema RPF itafanya kampeni nchini kote na kuwafahamisha wananchi wa Rwanda mipango yake katika miaka saba ijayo.

Kampeni za uchaguzi zitaanza rasmi kesho hadi tarehe 3 mwezi ujao wilayani Ruhango, mkoa wa Kusini.

Exit mobile version