Chelsea yakiona cha moto ndani ya Stadio Olimpico.

In Kimataifa, Michezo

Chelsea wakicheza ugenini katika uwanja wa Stadio Olimpico, wamepokea kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa wababe wa Italia As Roma, katika mchezo wa ligi ya klabu bingwa barani Ulaya uliopigwa jana usiku.

Sekunde 39 tu baada ya mchezo huo kuanza Stephan El Shaarawy aliwapatia Roma bao la kuongoza, likiwa ni bao la haraka zaidi kuwahi kufungwa katika michuano ya klabu bingwa.

El Shaarawy aliongeza bao la pili kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza, baada ya makosa ya beki wa zamani wa As Roma Antonio Rudiger huku Diego Perotti akipachika bao la tatu dakika ya 63 na kuifanya Roma kupata ushindi wa mabao 3-0.

Hii ni kama historia kujirudia kwani mwaka 2008 Chelsea wakicheza katika uwanja wa Stadio Olimpico walipata kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa As Roma.

Cesc Fabregas amekuwa mchezaji wa tano kucheza michezo 100 ya champions league akiwa na umri mdogo, ambapo katika mchezo dhidi ya As Roma alikuwa na miaka 30 na siku 180.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu