Chelsea yakiona cha moto ndani ya Stadio Olimpico.

In Kimataifa, Michezo

Chelsea wakicheza ugenini katika uwanja wa Stadio Olimpico, wamepokea kipigo cha mabao 3-0 kutoka kwa wababe wa Italia As Roma, katika mchezo wa ligi ya klabu bingwa barani Ulaya uliopigwa jana usiku.

Sekunde 39 tu baada ya mchezo huo kuanza Stephan El Shaarawy aliwapatia Roma bao la kuongoza, likiwa ni bao la haraka zaidi kuwahi kufungwa katika michuano ya klabu bingwa.

El Shaarawy aliongeza bao la pili kabla ya kumalizika kwa kipindi cha kwanza, baada ya makosa ya beki wa zamani wa As Roma Antonio Rudiger huku Diego Perotti akipachika bao la tatu dakika ya 63 na kuifanya Roma kupata ushindi wa mabao 3-0.

Hii ni kama historia kujirudia kwani mwaka 2008 Chelsea wakicheza katika uwanja wa Stadio Olimpico walipata kipigo cha mabao 3-1 kutoka kwa As Roma.

Cesc Fabregas amekuwa mchezaji wa tano kucheza michezo 100 ya champions league akiwa na umri mdogo, ambapo katika mchezo dhidi ya As Roma alikuwa na miaka 30 na siku 180.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu