Christian Democratic Union CDU kimekishinda chama cha Social Democrats SPD katika uchaguzi wa jimbo la North Rhine Westphalia ambayo ni ngome ya SPD.

In Kimataifa

Chama cha Kansela wa Ujerumani Angela Merkel cha Christian Democratic Union CDU kimekishinda kile cha Social Democrats SPD katika uchaguzi wa jimbo la North Rhine Westphalia ambayo ni ngome ya SPD.
Matokeo ya awali yanaonyesha CDU kimeshinda uchaguzi huo uliofanyika jana Jumapili kwa asilimia 33 huku SPD ambacho kimeliongoza jimbo hilo kwa karibu nusu karne kikiibuka katika nafasi ya pili kwa asilimia 31.3 na chama cha Free Democratic Party FDP kinachonuia kurejea katika bunge la Ujerumani kikiwa katika nafasi ya tatu kwa asilimia 12.5 ya kura.
Ushindi huo wa CDU umeongeza matumaini ya Merkel kusalia madarakani kwa muhula wa nne katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Septemba mwaka huu.
Mgombea Ukansela wa SPD Martin Schulz amesema matokeo hayo ni pigo kubwa kwa chama chake na kwake binafsi.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Schulz amesema wameshindwa vibaya katika jimbo analotokea. Asilimia 65. 2 ya watu walio na haki ya kupiga kura walishiriki uchaguzi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu