Christian Democratic Union CDU kimekishinda chama cha Social Democrats SPD katika uchaguzi wa jimbo la North Rhine Westphalia ambayo ni ngome ya SPD.

In Kimataifa

Chama cha Kansela wa Ujerumani Angela Merkel cha Christian Democratic Union CDU kimekishinda kile cha Social Democrats SPD katika uchaguzi wa jimbo la North Rhine Westphalia ambayo ni ngome ya SPD.
Matokeo ya awali yanaonyesha CDU kimeshinda uchaguzi huo uliofanyika jana Jumapili kwa asilimia 33 huku SPD ambacho kimeliongoza jimbo hilo kwa karibu nusu karne kikiibuka katika nafasi ya pili kwa asilimia 31.3 na chama cha Free Democratic Party FDP kinachonuia kurejea katika bunge la Ujerumani kikiwa katika nafasi ya tatu kwa asilimia 12.5 ya kura.
Ushindi huo wa CDU umeongeza matumaini ya Merkel kusalia madarakani kwa muhula wa nne katika uchaguzi mkuu unaotarajiwa mwezi Septemba mwaka huu.
Mgombea Ukansela wa SPD Martin Schulz amesema matokeo hayo ni pigo kubwa kwa chama chake na kwake binafsi.
Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Schulz amesema wameshindwa vibaya katika jimbo analotokea. Asilimia 65. 2 ya watu walio na haki ya kupiga kura walishiriki uchaguzi huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu