Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona nchini Kenya imeongezeka hadi 672 baada ya wagonjwa wapya 23 kukutwa na virusi hivyo katika kipindi cha saa 24.
Wakati wa mkutano na waandishi wa habari siku ya Jumapili katibu msimamizi wa maswala ya Afya nchini Kenya Rashid Aman amesema kuwa idadi ya waliopona virusi yafika 239 baada ya wagonjwa wengine 32 kupona virusi hivyo.
Kati ya idadi hiyo wagonjwa 12 wameripotiwa kutoka Mombasa , sita kutoka Mandera wanne kutoka Nairobi na mmoja kutoka Kajiado.
Dkt Aman amesema kwamba wagonjwa watatu wa;likuwa wakitoka katika vifaa vya karantini.
Amsema kwamba sampuli 32,097 zilifanyiwa vipimo nchini kufikia sasa.
Ili kuzuia kusambaa kwa virusi hivyo , serikali imewaagiza madereva wote wa malori ya masafa marefu kufanyiwa vipimo vya lazima saa 48 kabla ya kuanza safari zao.
