Dar es salaam siyo sehemu ya kuzalisha uhalifu MAMBOSASA

Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amesema atahakikisha anakataa Dar es Salaam kuwa maficho ya watu wanaofanya uhalifu maeneo ya pembezoni na kukimbilia jijini humo na kubaki salama, pamoja na kuhakikisha jiji hilo siyo sehemu ya kuzalisha uhalifu.

Aidha, amewaomba wananchi wote wa Mkoa wa Dar es Salaam pamoja na waandishi wa habari, kumpatia ushirikiano wa kutosha ili kukabiliana na uhalifu na kuifanya jamii kuishi katika hali ya amani na usalama.

Akizungumza na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe kuwa kamanda wa kanda hiyo, Mambosasa alisema usalama wa jiji hilo unawezekana, endapo wananchi watatoa ushirikiano na kuacha kufumbia macho wahalifu, badala yake kuripoti matukio ya uhalifu kwa wakati.

Hata hivyo amesema kuwa  hawezi kukubali Dar es Salaam ikawa ni sehemu ya watu kukimbilia baada ya kufanya uhalifu au kufanya uhalifu na kukimbilia maeneo ya pembezoni.

 

 

 

 

 

Exit mobile version