Diva ang’atuka Clouds media

In Kitaifa

Mtangazaji maarufu wa kipindi cha Ala za Roho cha Clouds FM, Diva the Boss ametangaza rasmi kuacha kazi katika kituo hicho baada ya kukitumikia kwa miaka 11 mfurulizo.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Diva ameandika; “Mashabiki wangu wa #AalaZaRoho mambo vipi? Mimi mwenyewe kwa akili zangu binafsi maamuzi yangu binafsi nachukua nafasi hii kuwaaga, nitawa-miss sana.

“Tumekuwa wote kwa miaka 11, worth it, natoa shukran zangu kwa uongozi wa Clouds FM kwa kunilea, Im forever thankful, shukrani kwa Joseph Kusaga na familia yake for making My Journey, ntakushukuruni sana.

“Positively nimeamua mwenyewe kuacha kazi Clouds FM leo (jana) mchana huu kwa mdomo wangu mbele ya HR na shahidi wake nilipotamka maneno hayo ya maamuzi ambayo toka natoka nyumbani nilisema nitafanya sababu ya vitu vingi tu ambavyo sitasema.

“Nashukuru sana sana sana, I’v been raised to be honest and speak up no matter what, sababu ya kusimamia ukweli wangu nimeamua fanya maamuzi ambayo nahisi ni sahihi kwangu… By saying That Life has a lot to offer Mungu yu Mwema… tutajuzana zaidi my next destination, love You all 💕,” ameandika Diva.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu