Diwani Vitimaalum aendesha Harambee kujenga Zahanati.

Diwani wa viti Maalumu CHADEMA Mhe.Digna John Nassari ameongoza harambee ya kujenga zahanati ya kijiji cha Nsengonyi kilichopo katika kata ya King’ori Jimbo la Arumeru Mashariki.

Harambee hiyo ya ujenzi wa Zahanati iliandaliwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Nsengonyi Ndg.Kanankira Peter Mafie pamoja na kamati ya Serikali ya Kijiji.

Mhe.Digna aliongozana na Diwani wa King’ori Mhe.Peter Kessi, Mhe.Wilson Nanyaro Diwani wa Nkoanekoli pamoja na diwani wa viti maalumu Mhe.Eva Julias Kaaya, Katika harambee hiyo kijijini hapo, wananchi walijitokeza kwa wingi kuchangia ujenzi huo wa zahanati kutokana na changamoto wazipatazo wanakijiji hao.

Akiongea katika harambee hiyo Mhe.Digna  alisema Zahanati hiyo itakayojengwa itawasaidia watu wote waishio kijijini hapo hasa kina Mama wajawazito ambapo huduma ya kujifungua inawalazimu kusafiri hadi kibong’oto Wilayani Siha.

Mwenyekiti wa Kijiji hicho pamoja na Kamati yake walisoma jumla ya fedha zilizopatikana katika harambee hiyo ambapo ilipatikana keshi na ahadi kiasi cha Pesa za kitanzania Shilingi Milioni 7,390,000,Pia Diwani wa Kata hiyo Mhe.Kessi alitoa kifaa cha Mahabara aina ya Microscope chenye thamani ya Shilingi 3,500,000.

 

Exit mobile version