Donald Ngoma kurudi uwanjani Kesho kuvaana na Waarabu

In Michezo
Baada ya kuwa nje ya uwanja kwa takriban mwezi mzima mshambuliaji wa Yanga, Mzimbabwe Donald Ndombo Ngoma amerejea kwenye kikosi hicho na yupo fiti kucheza mbele ya Waarabu MC Alger ya Algeria kwenye mechi ya Kombe la shirikisho
Daktari wa Yanga, Edward Bavu amesema  Ngoma ana asilimia 100 za kucheza mchezo huo kwani yuko fiti na kwamba ana zaidi ya wiki mbili tangu apone ambapo alikuwa akifanya mazoezi madogo madogo na timu.
“Sina shaka tena na hali ya Ngoma ambaye alikuwa  akisumbuliwa na maumivu ya mguu tayari amesharejea uwanjani na kwamba ana uhakika wa kuwavaa  MC Alger kesho kwani hali yake kwa jumla inaridhisha sana na kwamba amepata muda mrefu wa kufanya mazoezi na wenzake.” Alisema Bavu
Ngoma amekuwa akiandamwa na majeraha ya mara kwa mara tangu ulipoanza mzunguko wa lala salama wa Ligi Kuu Tanzania Bara kiasi cha kumfanya ashindwe kuitumikia klabu yake ya Yanga kwenye michezo muhimu mbalimbali iliyokuwa mbele yao ukiwemo ule dhidi ya Simba ambao waliolala mabao 2-1.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu