Donald Ngoma kurudi uwanjani Kesho kuvaana na Waarabu

In Michezo
Baada ya kuwa nje ya uwanja kwa takriban mwezi mzima mshambuliaji wa Yanga, Mzimbabwe Donald Ndombo Ngoma amerejea kwenye kikosi hicho na yupo fiti kucheza mbele ya Waarabu MC Alger ya Algeria kwenye mechi ya Kombe la shirikisho
Daktari wa Yanga, Edward Bavu amesema  Ngoma ana asilimia 100 za kucheza mchezo huo kwani yuko fiti na kwamba ana zaidi ya wiki mbili tangu apone ambapo alikuwa akifanya mazoezi madogo madogo na timu.
“Sina shaka tena na hali ya Ngoma ambaye alikuwa  akisumbuliwa na maumivu ya mguu tayari amesharejea uwanjani na kwamba ana uhakika wa kuwavaa  MC Alger kesho kwani hali yake kwa jumla inaridhisha sana na kwamba amepata muda mrefu wa kufanya mazoezi na wenzake.” Alisema Bavu
Ngoma amekuwa akiandamwa na majeraha ya mara kwa mara tangu ulipoanza mzunguko wa lala salama wa Ligi Kuu Tanzania Bara kiasi cha kumfanya ashindwe kuitumikia klabu yake ya Yanga kwenye michezo muhimu mbalimbali iliyokuwa mbele yao ukiwemo ule dhidi ya Simba ambao waliolala mabao 2-1.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu