DTG kuanza kutumika Kenya kwa mara ya kwanza.

In Kimataifa
Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika, kuanza kutumia dawa mpya ya kupambana na virusi vya Ukimwi inayofahamika kama DTG.
Dawa hiyo mpya inayosaidia mwathirika kuendelea kuishi kwa muda mrefu, ilitengenezwa na kuidhinishwa na Marekani mwaka 2013.
Watalaam wamesema waathiriwa zaidi ya 20,000 nchini Kenya wanapewa dawa hiyo kuona matokeo yake  na baadaye itakwenda nchini Nigeria na hatimaye  nchini Uganda.
Doughtiest Ogutu, mmoja wa watumizi wa dawa hiyo mpya, ameliambia Shirika la Habari la Reuters kuwa ameamua kutumia hiyo mpya kwa sababu dawa nyingine aliyokuwa anatumia ilikuwa haimsaidii.
Kenya ni miongoni mwa mataifa ya Afrika yanayoendelea kukabiliwa na janga la maambukizi ya Ukimwi.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na maambukizi ya Ukimwi UNAIDS, linalenga kuwa ifikapo mwaka 2020, asilimia 90 ya waathiriwa wa virusi hivyo watakuwa wameanza kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu