DTG kuanza kutumika Kenya kwa mara ya kwanza.

In Kimataifa
Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika, kuanza kutumia dawa mpya ya kupambana na virusi vya Ukimwi inayofahamika kama DTG.
Dawa hiyo mpya inayosaidia mwathirika kuendelea kuishi kwa muda mrefu, ilitengenezwa na kuidhinishwa na Marekani mwaka 2013.
Watalaam wamesema waathiriwa zaidi ya 20,000 nchini Kenya wanapewa dawa hiyo kuona matokeo yake  na baadaye itakwenda nchini Nigeria na hatimaye  nchini Uganda.
Doughtiest Ogutu, mmoja wa watumizi wa dawa hiyo mpya, ameliambia Shirika la Habari la Reuters kuwa ameamua kutumia hiyo mpya kwa sababu dawa nyingine aliyokuwa anatumia ilikuwa haimsaidii.
Kenya ni miongoni mwa mataifa ya Afrika yanayoendelea kukabiliwa na janga la maambukizi ya Ukimwi.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na maambukizi ya Ukimwi UNAIDS, linalenga kuwa ifikapo mwaka 2020, asilimia 90 ya waathiriwa wa virusi hivyo watakuwa wameanza kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

NACTIVET YASIMAMISHA MAFUNZO CHUO CHA MBEYA TRAINING..DC MALISA AAGIZA KUFANYIWA UHAKIKI VYUO VYOTE WILAYA YA MBEYA

Wazazi Wanafunzi na wahitimu wa chuo cha Mbeya training wameiomba serikali iwasaidie kurudishiwa stahiki zao mara baada ya kubainika

Read More...

TETESI ZA SOKA ULAYA LEO JUMANNE NOVEMBA 7, 2023

Manchester United na Newcastle United zote zinamfuatilia mshambuliaji wa Lyon Mfaransa Rayan Cherki, 20, ambaye mkataba wake unamalizika Juni

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu