DTG kuanza kutumika Kenya kwa mara ya kwanza.

In Kimataifa
Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika, kuanza kutumia dawa mpya ya kupambana na virusi vya Ukimwi inayofahamika kama DTG.
Dawa hiyo mpya inayosaidia mwathirika kuendelea kuishi kwa muda mrefu, ilitengenezwa na kuidhinishwa na Marekani mwaka 2013.
Watalaam wamesema waathiriwa zaidi ya 20,000 nchini Kenya wanapewa dawa hiyo kuona matokeo yake  na baadaye itakwenda nchini Nigeria na hatimaye  nchini Uganda.
Doughtiest Ogutu, mmoja wa watumizi wa dawa hiyo mpya, ameliambia Shirika la Habari la Reuters kuwa ameamua kutumia hiyo mpya kwa sababu dawa nyingine aliyokuwa anatumia ilikuwa haimsaidii.
Kenya ni miongoni mwa mataifa ya Afrika yanayoendelea kukabiliwa na janga la maambukizi ya Ukimwi.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalopambana na maambukizi ya Ukimwi UNAIDS, linalenga kuwa ifikapo mwaka 2020, asilimia 90 ya waathiriwa wa virusi hivyo watakuwa wameanza kutumia dawa za kupunguza makali ya ugonjwa huo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu