Federer amshinda Nadal Shangai Masters.

In Kimataifa, Michezo

Bingwa mtetezi wa Wimbledon Roger Federer amemshinda mchezaji namba moja kwa ubora duniani Rafael Nadal kwa seti 6-4 6-3 katika michuano ya Shanghai na kuwa kikombe chake cha sita kwa mwaka huu.
Federer ambaye amepoteza michezo minne tu kwa mwka 2017, alikuwa katika kiwango cha juu na kushinda ndani ya dakika 72.
Ulikuwa ushindi wake wa nne kwa mwaka huu dhidi ya Nadal na wa sita mfululizo.
Federer ameshinda mataji 94 katika maisha yake ya uchezaji tenisi huku 19 ikiwa ni grand slam.
Inamfanya kufikia rekodi ya Ivan Lendl wakipitwa na Jimmy Connors wa Marekani mwenye vikombe 109.
Icardi aiongoza Inter Millan kuilaza Ac Millan…
Inter Millan waliibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya wapinzai wao wa jadi Ac Millan katika mchezo wa ligu ya Italia Serie A huku mshambuliaji Mauro Icardi ambaye ni nahodha wa klabu hiyo akipiga Hat-trick katika mchezo huo.
Dakika 28 tu za mwanzo Icardi alionesha makucha yake baada ya kufunga bao la kwanza lililodumu hadi mapumziko, lakini Ac Millan walirudi kipindi cha pili na kusawazisha kupitia kwa Susso.
Mauro Icardi tena dakika ya 68 aliongeza la pili kabla ya Millan kuchomoa dakika ya 81 kupitia kwa Giacomo Bonaventura na wakaamini mpira unaweza isha kwa suluhu lakini Icardi tena dakika ya 90 akafunga bao kwa mkwaju wa penati na kuifanya Inter Millan kushinda 3-2.
Kwa matokeo hayo sasa Ac Millan wanashika nafasi ya 10 na alama zao 12 huku Inter Millan wakibaki katika nafasi yao ya pili wakiwa wamejikusanyia alama 22 msimu huu.
Mchezo huo ulikuwa na msisimko wa kipekee ukihudhuliwa na mashabiki wengi kutokana na uwekezaji mpya ulifanywa na timu zote mbili zinazomilikiwa na wawekezaji kutoka China.
Jose Mourinho asema hatastaafu akiwa Man Utd…
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho amesema haamini kwamba atastaafu ukufunzi akiwa bado katika klabu hiyo ya Ligi ya Premia.
Mreno huyo wa miaka 54 ambaye kwa sasa anahudumu kwa msimu wake wa pili kama mkufunzi Old Trafford hajawahi kukaa zaidi ya miaka minne katika klabu moja.
Amefanya kazi katika jumla ya klabu saba.
Akiongea na runinga moja ya Ufaransa, Mourinho alisema anafikiri kwamba Paris St-Germain ni klabu nzuri sana.
Mkufunzi huyo wa zamani wa Chelsea, Real Madrid, Inter Milan na Porto aliambia kipindi cha Telefoot cha TF1 kwamba: “Siamini, hapana, sina uhakika kwamba nitafikisha kikomo ukufunzi wangu hapa.”
Mourinho, aliyeshinda Kombe la EFL na Europa League msimu wake wa kwanza Old Trafford, amesema mtoto wake wa kiume amekuwa akitazama mechi za PSG sana karibuni.
Mkataba wa Mourinho kwa sasa ni wa miaka mitatu na anaweza kuongezewa mkataba huo hivyo basi anaweza kusalia United hadi 2020.
Awali hata hivyo amewahi kudokeza kwamba angependa kukaa United kwa muda mrefu.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu