Fenerbahce wanamtaka mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa.

In Kimataifa, Michezo

Klabu ya Fenerbahce ya Uturuki imefanya mazungumzo na wawakilishi wa mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa kuhusu uwezekano wa kumchukua kwa mkopo.

Costa, 28, amesalia nchini Brazil na amekataa kurejea England.

Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uhispania alishindwa kuhama kutoka kwa mabingwa hao wa Ligi ya Premia kabla ya siku ya mwisho ya kuhama wachezaji katika ligi nyingi kuu Ulaya.

Hata hivyo, dirisha la uhamisho wa wachezaji Uturuki bado liko wazi na litafungwa baadaye leo Ijumaa.

Duru zinasema baada ya mazungumzo ya kwanza kufanyika, uwezekano wake kuhama ni finyu, lakini mazungumzo bado yanaendelea.

Costa ameambia na meneja wa Chelsea Antonio Conte ajitafutie klabu itakayomchukua.

Alitaka kurejea Atletico Madrid majira ya joto lakini klabu hiyo ya Uhispania hairuhusiwi kuwasajili wachezaji kutokana na marufuku waliyowekewa hadi Januari.

Hii ina maana kwamba Costa anaweza tu kuhamia klabu hiyo Januari mwakani.

Mshambuliaji huyo hajajumuishwa kwenye orodha ya wachezaji wa Chelsea watakaoshiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

ZOEZI LA UOKOAJI HANANG, MAWAZIRI WAFIKA

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Mhe. Jenista J. Mhagama, Waziri wa Ujenzi Innocent

Read More...

RC MBEYA AFANYA UZINDUZI ZOEZI LA UGAWAJI VITAMBULISHO VYA (NIDA)

Mkuu wa mkoa wa mbeya Mhe. Comrede Juma Zuberi Homera amefanya uzinduzi wa wa zoezi la ugawaji wa vitambulisho

Read More...

MAADHIMISHO YA WATOTO DUNIANI YAFANYIKA ARUSHA

Siku ya watoto duniani kitaifa imeazimishwa hapa jiji Arusha katika hoteli ya mount meru na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu