Gharama ya Zika ni hadi dola bilioni 18 kwa miaka mitatu ijayo.

In Kimataifa

Tathmini mpya kuhusu ugonjwa wa Zika kwa nchi za Amerika ya Kusini imeonyesha kuwa athari za kijamii na kiuchumi zitokanazo na ugonjwa huo zitakuwa za muda mrefu zaidi kuliko ilivyotarajiwa.

Ikifanywa kwa ushirikiano kati ya shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP na shirikisho la msalaba na hilal nyekundu, IFRC, tathmini hiyo imeonyesha kuwa Zika itagharimu nchi hizo kati ya dola bilioni 7 hadi 18 kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Brazil ndiyo itakayobeba mzigo zaidi kwa kuwa Zika inasababisha watalii kupungua na hivyo mapato ya kiuchumi kushuka.

Kwa kuzingatia athari mtambuka za Zika, serikali zimetakiwa kupanga bajeti zao ipasavyo badala ya kujikita tu katika kuimarisha huduma za afya na wakati huo huo kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa kama homa ya dengue, manjano na chikingunya ambayo yote huenezwa na mbu aina ye Aedes anayesambaza pia virusi vya Zika.

Katika kupanga bajeti, serikali zimetakiwa kujumuisha wadau mbali mbali ikwemo jamii, mashirika ya kiraia na sekta binafsi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu