Gharama ya Zika ni hadi dola bilioni 18 kwa miaka mitatu ijayo.

In Kimataifa

Tathmini mpya kuhusu ugonjwa wa Zika kwa nchi za Amerika ya Kusini imeonyesha kuwa athari za kijamii na kiuchumi zitokanazo na ugonjwa huo zitakuwa za muda mrefu zaidi kuliko ilivyotarajiwa.

Ikifanywa kwa ushirikiano kati ya shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP na shirikisho la msalaba na hilal nyekundu, IFRC, tathmini hiyo imeonyesha kuwa Zika itagharimu nchi hizo kati ya dola bilioni 7 hadi 18 kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo.

Brazil ndiyo itakayobeba mzigo zaidi kwa kuwa Zika inasababisha watalii kupungua na hivyo mapato ya kiuchumi kushuka.

Kwa kuzingatia athari mtambuka za Zika, serikali zimetakiwa kupanga bajeti zao ipasavyo badala ya kujikita tu katika kuimarisha huduma za afya na wakati huo huo kuimarisha kinga dhidi ya magonjwa kama homa ya dengue, manjano na chikingunya ambayo yote huenezwa na mbu aina ye Aedes anayesambaza pia virusi vya Zika.

Katika kupanga bajeti, serikali zimetakiwa kujumuisha wadau mbali mbali ikwemo jamii, mashirika ya kiraia na sekta binafsi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

JUMLA YA WATU 2249 VISIWA VYA MULEBA WAPATIWA ELIMU YA UGONJWA WA MARBURG .

Baadhi ya Watalaam wa Afya kutoka Wizara ya Afya wakitoa Elimu katika kisiwa Cha Rushonga kilichopo ndani ya ziwa

Read More...

MAANDALIZI DIRA YA MAENDELEO 2050 YAANZA

SERIKALI  imeanza mchakato Wa kuandaa Dira Mpya ya Maendeleo 2050 ambapo wadau wote katika maeneo yao wametakiwa kushiriki kikamilifu

Read More...

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu