Goodbless Lema ametoa shukrani zake kwa Mbunge, Lazaro Nyalandu

In Kitaifa

Mbunge wa Arusha Mjini,  Goodbless Lema ametoa shukrani zake kwa Mbunge, Lazaro Nyalandu kwa kufanikisha safari ya Marekani ya watoto  watatu, ambao walinusurika kifo katika ajali ya basi la shule ya Lucky Vicent iliyotokea Karatu na kusababisha vifo vya watu 35

Lema amesema tangu kutokea kwa Ajali hiyo mbunge huyo amekuwa akionesha ushirikiano mkubwa jambo ambalo linastahili kupongezwa.

Aidha, tangu itokee ajali hiyo, Nyalandu amekuwa bega kwa bega na kufuatilia kila hatua, ili kuhakikisha watoto hao pamoja na wazazi wao na daktari wanasafiri kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kupata matibabu zaidi.

Katika hatua nyingine, Nyalandu ameomba pesa zitakazo endelea kuchangwa na Watanzania na watu wengine duniani kwa ajili ya watoto hao zitumike kujenga ICU katika hospitali ya Mount Meru ambayo itakuwa ni msaada mkubwa kwa wakazi wa Arusha na mikoa jirani pindi linapotokea tatizo kama hilo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu