Goodbless Lema ametoa shukrani zake kwa Mbunge, Lazaro Nyalandu

In Kitaifa

Mbunge wa Arusha Mjini,  Goodbless Lema ametoa shukrani zake kwa Mbunge, Lazaro Nyalandu kwa kufanikisha safari ya Marekani ya watoto  watatu, ambao walinusurika kifo katika ajali ya basi la shule ya Lucky Vicent iliyotokea Karatu na kusababisha vifo vya watu 35

Lema amesema tangu kutokea kwa Ajali hiyo mbunge huyo amekuwa akionesha ushirikiano mkubwa jambo ambalo linastahili kupongezwa.

Aidha, tangu itokee ajali hiyo, Nyalandu amekuwa bega kwa bega na kufuatilia kila hatua, ili kuhakikisha watoto hao pamoja na wazazi wao na daktari wanasafiri kwenda nchini Marekani kwa ajili ya kupata matibabu zaidi.

Katika hatua nyingine, Nyalandu ameomba pesa zitakazo endelea kuchangwa na Watanzania na watu wengine duniani kwa ajili ya watoto hao zitumike kujenga ICU katika hospitali ya Mount Meru ambayo itakuwa ni msaada mkubwa kwa wakazi wa Arusha na mikoa jirani pindi linapotokea tatizo kama hilo.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu