Hakuna kijiji kitasalia bila kuunganishwa umeme. Waziri Mkuu

In Kitaifa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema hakuna kijiji nchini kitakachoachwa bila ya kuunganishiwa umeme katika awamu ya tatu ya mradi unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (Rea).

Amesema Serikali imetenga Sh trilioni moja kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 8,000, ambavyo bado havijaunganishiwa na nishati hiyo.

Amesema hayo katika mikutano aliyoifanya kwenye vijiji vya Chiapi, Nandanga, Mbecha na Luchelegwa, ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Lindi.

Waziri mkuu amesema kuwa gharama za kulipa umeme huo ni shilingi elfu 27 tu, ambapo  wananchi hawatawajibika kulipia nguzo na fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme, kwa sababu tayari gharama hizo zimebebwa na Serikali.

Amesema lengo la Serikali ni kufikisha umeme kwenye vijiji vyote Tanzania na kwa vile ambavyo viko kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi ya Taifa, vitafungiwa umeme Jua (sola), hivyo kufungua fursa za Ajira na kukuza uchumi.

Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Lindi, Johnson Mwigune amesema hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu, mkandarasi aliyepangwa kufanya kazi katika vijiji hivyo atakuwa ameanza kusambaza umeme.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Maagizo ya wizara kuhusu mfuko wa maendeleo ya kilimo.

Naibu Waziri Wa Kilimo Anthony Mavunde, amesema serikaliimeanza kutekeleza uanzishwaji wa mfuko wa maendeleo yakilimo utakaosaidia kukabiliana na changamoto

Read More...

TANZIA: WAZIRI MSTAAFU WA KILIMO AFARIKI DUNIA

Aliyewahi kuwa mbunge wa jimbo la Musoma Vijijini na Waziri wa Kilimo na Mifugo Mhe. Herman Kirigini Amefariki Dunia. Akithibitisha

Read More...

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Professor Makame Mbarawaameliomba Bunge kumuidhinishia kiasi cha Sh Trilioni 3.6ikiwa ni makadirio ya mapato

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu