Hakuna kijiji kitasalia bila kuunganishwa umeme. Waziri Mkuu

In Kitaifa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema hakuna kijiji nchini kitakachoachwa bila ya kuunganishiwa umeme katika awamu ya tatu ya mradi unaotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijini (Rea).

Amesema Serikali imetenga Sh trilioni moja kwa ajili ya kusambaza umeme katika vijiji 8,000, ambavyo bado havijaunganishiwa na nishati hiyo.

Amesema hayo katika mikutano aliyoifanya kwenye vijiji vya Chiapi, Nandanga, Mbecha na Luchelegwa, ikiwa ni siku ya pili ya ziara yake ya kikazi ya siku nne mkoani Lindi.

Waziri mkuu amesema kuwa gharama za kulipa umeme huo ni shilingi elfu 27 tu, ambapo  wananchi hawatawajibika kulipia nguzo na fomu za maombi ya kuunganishiwa umeme, kwa sababu tayari gharama hizo zimebebwa na Serikali.

Amesema lengo la Serikali ni kufikisha umeme kwenye vijiji vyote Tanzania na kwa vile ambavyo viko kwenye maeneo yaliyo mbali na gridi ya Taifa, vitafungiwa umeme Jua (sola), hivyo kufungua fursa za Ajira na kukuza uchumi.

Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) Mkoa wa Lindi, Johnson Mwigune amesema hadi kufikia mwishoni mwa mwezi huu, mkandarasi aliyepangwa kufanya kazi katika vijiji hivyo atakuwa ameanza kusambaza umeme.

 

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu