Halmashauri kuu ya CCM yakutana kupitisha wagombea.


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM Rais John Pombe
Magufuli, amesema kamati ya maadili na usalama na kamati kuu
ya CCM zilipitia majina yote zaidi ya 10,000 ya wana CCM
walioomba kuteuliwa kugombea ubunge ili kuhakikisha hakuna
atakayeonewa.


Amesema CCM ni chama kinachopendwa na hii ni kutokana na
watu wa aina zote waliojitokeza kuomba nafasi mbalimbali na
kufikia takribani elfu 43, ambapo amesema inawezekana chama
hicho kimevyunja rekodi hata Afrika baada ya watu wengi
kujitokeza kuomba nafasi za kugombea.


Rais Magifuli ameyasea hayo alipokuwa akifungua rasmi kikao
cha hamashauri kuu ya CCM,yenye dhamana ya kuwapitisha
wagombea wataopeperusha bendera ya chama hicho katika
uchaguzi mku wa mwezi October.

Baada ya hotuba fupi ya Rais Magufuli katibu wa itikadi na
uenezi wa CCM Humphrey Polepole, akatangaza majina ya

wagombea ubunge wa CCM waliopitishwa na Kamati ya
halmashauri kuu ya Taifa ya chama hicho.

Exit mobile version