Halmashauri ya jiji la Arusha imetoa mkopo wa Shilingi bilioni 1.3, kwa ajili ya wakinamama na vijana wa kwa lengo la kutimiza adhma ya raisi John Pombe Magufuli ya kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira ,na kuweza kuinua kipato cha wananchi kwa kunufaika na miradi mbalimbali na hatimae kuweza kujikwamua kiuchumi.

In Kitaifa

Halmashauri ya jiji la Arusha imetoa mkopo wa Shilingi bilioni 1.3,  kwa ajili ya wakinamama na vijana wa kwa lengo la kutimiza adhma ya raisi John Pombe Magufuli ya kutatua changamoto ya ukosefu wa ajira ,na kuweza kuinua kipato cha wananchi kwa kunufaika na miradi mbalimbali na hatimae kuweza kujikwamua kiuchumi.

Mkuu wa Idara ya Maendeleo ya jamii  Janeth Masasi   amesema   kuwa vikundi vya  wanawake vimepokea kiasi cha shilingi  milioni 390 ,huku vikundi vya vijana vimekabidhiwa shilingi milioni 336 .Hata hivyo amesema kuwa mikopo hiyo itasaidia katika uanzishwaji wa viwanda vidogo vidogo ,ambavyo vitasaidia kutengeneza ajira na kukuza uchumi

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Gabriel Daqqaro amesema kuwa kutokana na changamoto iliyoko  katika taasisi za fedha, ambazo hutoa mikopo kwa riba kubwa na kuhitaji dhamana ya nyumba na adhi jambo ambalo linawakwamisha wakopaji hivyo serikali imeamua kutoa mikopo ya masharti nafuu.Aidha amesema mikopo  hiyo itawasaidia makundi hayo kuweza  kuongeza mitaji na kutoa ajira ndani ya jamii.

Kwa upande wao kinamama na Vijana waliopokea mikopo hiyo wamesema kuwa mikopo hiyo itawainua kiuchumi, na kuwawezesha kufanya shughuli za uzalishaji mali na kuachana na matumizi ya dawa za kulevya  pamoja na wizi.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu