Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo sasa kutoa wataalam.

In Kitaifa
Serikali imesema kuwa itashirikiana na Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo katika kutoa wataalam, kuandaa michoro na kusimamia ujenzi wa barabara  zote zinazoingia katika viwanda vinavyojengwa mkoani Pwani.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Eng. Edwin Ngonyani, amesema kuwa hatua hiyo imefikiwa mara baada ya uongozi wa Halmashauri ya wilaya hiyo kuandika barua kwa Wizara hiyo kuomba msaada wa kujengewa barabara ya Km 1 inayoingia kwenye kiwanda kipya cha Matunda  cha Sayona kutoka kwenye barabara kuu ya Chalinze – Arusha na ile iliyopo katika kiwanda cha kutengeneza marumaru na masinki cha Twyford.
Aidha, Naibu Waziri huyo ameutaka uongozi wa Halmashauri hiyo kutumia fedha za Bodi ya Mfuko wa Barabara (RFB), kuona namna ya kujenga barabara hizo na kuhakikisha ubora wa barabara hizo unaendana na thamani ya fedha zinazotolewa.
Kuhusu ujenzi wa barabara inayoingia kwenye kiwanda cha kutengeneza marumaru na masinki kilichopo wilayani hapo, Naibu Waziri Ngonyani, ameuagiza uongozi wa TANROADS mkoani humo kupima na kufanya tathmini ya gharama za ujenzi wa barabara hiyo ili kupata taarifa sahihi.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Bagamoyo Bw. Magid Mwanga, ameipongeza Serikali ya Awamu ya Tano kwa kufanya kazi kwa vitendo kwa kuchukua hatua za haraka za kutembelea maeneo hayo na kuboresha miundombinu ya barabara katika viwanda ili kuhamasisha na kuchochea wawekezaji wa viwanda nchini.
Dhamira ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kujenga miundombinu bora kwa wananchi wake na Taifa kwa ujumla ili kuhamasisha uwekezaji wa viwanda na huduma za usafirishaji ili kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu