Harbinder Sethi, Rugemarila hadi 31 agosti 2017 Mahakamani.

In Kitaifa

 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo imeahirisha kesi ya kutakatisha fedha inayomkabili Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL Harbinder Singh Sethi, na James Rugemarila hadi August 31 2017 kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mfawidhi Cyprian Mkeha kuwa, upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba iahirishwe hadi tarehe nyingine.

Baada ya maelezo hayo ya wakili wa Swai, Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi August 31 2017 ambapo washtakiwa wamerudishwa rumande.

Harbinder Singh Sethi pamoja na Mfanyabiashara James Rugemarila, kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya zaidi ya Bilioni 3.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Tigo na mjasiriamali Boss yaja kukomboa wajasiriamali

Katika kuendelea kukuza utalii wa utamaduni hapa nchini kampuni ya Tigo kanda ya kaskazini imeendeleaa kuwaunga mkono wadau wa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu