Harbinder Sethi, Rugemarila hadi 31 agosti 2017 Mahakamani.

In Kitaifa

 

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, leo imeahirisha kesi ya kutakatisha fedha inayomkabili Mmiliki wa Kampuni ya kufua umeme ya IPTL Harbinder Singh Sethi, na James Rugemarila hadi August 31 2017 kutokana na upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika.

Mwendesha Mashtaka wa TAKUKURU Leornad Swai amemueleza Hakimu Mkazi Mfawidhi Cyprian Mkeha kuwa, upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika, hivyo anaomba iahirishwe hadi tarehe nyingine.

Baada ya maelezo hayo ya wakili wa Swai, Hakimu Mkeha aliahirisha kesi hiyo hadi August 31 2017 ambapo washtakiwa wamerudishwa rumande.

Harbinder Singh Sethi pamoja na Mfanyabiashara James Rugemarila, kwa pamoja wanakabiliwa na mashtaka 12 yakiwemo ya kutakatisha fedha na kuisababisha Serikali hasara ya zaidi ya Bilioni 3.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu