Hospitali kumi na sita nchini Uingereza zimeathirika kutokana na shambulio la programu ya virusi vya kompyuta hapo jana.

In Kimataifa

Hospitali kumi na sita nchini Uingereza zimeathirika kutokana na shambulio la programu ya virusi vya kompyuta hapo jana.

Hospitali kadhaa katika jiji la London na maeneo mengine mbalimbali nchini humo zililazimika kufunga mitambo yake ya kompyuta. Virusi hivyo kimsingi vinazuia watumiaji wa kopmyuta kupata data zao hadi walipe fidia.

Hata hivyo madaktari wamesema licha ya kompyuta hizo kushambuliwa na virusi, data za wagonjwa hazikupotea.

Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May amesema tukio hilo ni sehemu ya shambulio kubwa lililo athiri mashirika mengine duniani kote, huku kukiwa na ripoti za mashambulizi hayo ya kompyuta katika nchi zipatazo 100 ikiwa ni pamoja na Marekani, China, Urusi, Uhispania, Italia, Taiwan na Ujerumani

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu