Hotel zavunjwa Nigeria kudhibiti Corona.

Maafisa nchini katika jimbo lenye utajiri wa mafuta la Rivers nchini Nigeria wamevunja hoteli mbili kufuatia madai ya kukiuka sheria za kukaa nyumbani zilizowekwa kwa lengo la kudhibiti kusambaa kwa virusi vya corona.

Gavana wa jimbo hilo Nyesom Wike, ambaye alisimulia kuvunjwa kwa Hoteli ya Edemete Hotel na Prodest Home Jumapili, alisema kuwa waliofanya shughuli hiyo walikuka maagizo kwamba hoteli zinapaswa kufungwa.

Alisema kuwa watu waliopatikana na virusi vya corona walipatikana katika hoteli mbali mbali katika jimbo hilo. Lakini hakusema iwapo yeyote ambaye ana maambukizi ya Covid-19 amekuwa akiishi katika hoteli hizo mbili zilizovunjwa.

Exit mobile version