Ibrahimovic atajwa katika kikosi cha Man Utd.

In Kimataifa, Michezo

Mshambuliaji wa Manchester United Zlatan Ibrahimovic amejumuishwa katika kikosi cha timu hiyo kitakacho shiriki katika michuano ya klabu bingwa barani Ulaya katika ngazi ya makundi.

Ibrahimovic mwenye umri wa miaka 35 aliachwa na Man United baada ya kupata maumivu ya goti mwezi Aprili lakini amejiunga tena na klabu hiyo na atakuwa miongoni mwa wachezaji watakaounda kikosi kitakacho shiriki katika michuano ya UEFA.

Awali kocha wa Manchester United Jose Mourinho alionyesha kuwa Zlatan asingeweza kuwa katika kikosi chake kitakachoshiriki katika Michuano ya klabu bingwa ngazi ya makundi lakini Zlatan amepona mapema na ataungana na kikosi cha Man Utd.

”Sidhani kama tutakuwa naye katika ngazi ya makundi nafikiri anaweza kujiunga na timu katika ngazi ya mtoano akiwa amepona” alisema Jose Mourinho.

 

Msimu uliopita Ibrahimovic alifanikiwa kuifungia Man United jumla ya mabao 28 na kuiwezesha timu hiyo kushinda kombe la Europa league pamoja na kombe la EFL.

 

Man United wataanza michuano ya klabu bigwa kwa kuwavaa FC Basel tarehe 12 mwezi Septemba kabla ya kucheza na CSKA Moscow tarehe 27 mwezi Septemba na Benfica tarehe 18 mwezi Octoba.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu