Ipo Lugha 1 inayozungumzwa na watu 3 pekee Afrika.

In Kimataifa, Kitaifa

Katrina Esau anafanya kila jitihada kuhakikisha kuwa lugha yake asili, ambayo kwa sasa inazungumzwa na watu watatu pekee, haiangamii.

Bi Esauni 84, ni mmoja wa watu watatu walio hai, ambao wanazungumza kwa ufasaha lugha iitwayo N|uu, mojawapo ya lugha zinazozungumzwa nchini Afrika Kusini ya jamii ya San, ambao pia wanafahamika kama Bushmen.

Lugha ya N|uu inachukuliwa kama lugha asili ya taifa la Afrika Kusini.

Huku kukiwa hakuna hata mtu mmoja ambaye anaweza kuzungumza kwa ufasaha lugha hiyo isipokuwa watu wa familia yake, lugha hiyo imetambuliwa na Umoja wa Mataifa kama lugha iliyo katika hatari kubwa ya kuangamia.

Lugha kubwa sita inayozungumzwa nchini Afrika Kusini:

Zulu Asilimia 22.7%, Xhosa Asilimia 16%, Afrikaans Asilimia13.5%,Kiingereza Asilimia 9.6%, Setswana Asilimia 8% na Sesotho Asilimia 7.6%

Kwa ujumla Afrika Kusini ina luhga rasmi 11.

Kiingereza ndio lugha inayozungumzwa kwa wingi kama lugha rasmi na lugha ya kibiashara.

 

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Viwango vya maadili kwa viongoiz yaongezeka.

Imeelezwa kuwa viwango vya uzingatiwaji wa maadili kwa viongozi na watumishi wa umma nchini,vimeongezeka hadi kufikia asilimi 75.9 kwa

Read More...

Watu 193 wawekwa karantini kisa virusi vya Marburg.

Mganga Mkuu wa serikali Dkt Tumaini Nagu,amesema hakuna kisa kipya kilichoongezeka kuhusu vifo vilivyosababishwa na virusi vya Ugonjwa wa

Read More...

SERIKALI YAFANYA UWEKEZAJI MKUBWA KATIKA HUDUMA ZA HALI YA HEWA

SERIKALI kupitia Wizara ya Ujenzi na uchukuzi,isemema kuwa katika kuhakikisha wanakuwa na Taarifa za uhakika za Hali ya hewa

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu