ISIS yathibitisha kifo cha kiongozi wake.

In Kimataifa

Kundi la Islamic State Alhamisi limethibitisha kifo cha kiongozi wake Abu Hussein al-Hussein al-Quraishi na limemteua Abu Hafs al-Hashimi al-Quraishi kama kiongozi wake mpya, msemaji wa kundi hilo alisema katika sauti kwenye mtandao wa Telegram wa kundi hilo.

Limeonekana kuwa tangazo la kwanza rasmi la kundi hilo kuhusu hatma ya kiongozi wake tangu Rais Tayyip Erdogan wa Uturuki aliposema mwezi Aprili kwamba maafisa wa ujasusi wa Uturuki walimuua kiongozi huyo wa ISIS nchini Syria.

Kundi hilo lilipata nguvu mwaka 2014 wakati kiongozi wake wa wakati huo, Abu Bakr al-Baghdadi, alipotangaza eneo linalodhibitiwa na kundi hilo kuwa chini ya sheria kali za kiislamu.

Abu Hussein al-Hussein al-Quraishi alichukua uongozi wa ISIS mwezi Novemba mwaka 2022, baada ya mtangulizi wake kuuawa pia nchini Syria.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

Wazazi wahimizwa kuzingatia Elimu Mbeya.

Afisa Tarafa wa Sisimba John Mboya amewataka wazazi na walezi kata ya Itagano Jijini Mbeya kuzingatia suala la elimu

Read More...

PROF. NDALICHAKO AKIPONGEZA KIWANDA CHA MBOLEA CHA ITRACOM KWA UTEKELEZAJI SHERIA ZA KAZI

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Prof. Joyce Ndalichako amekipongeza kiwanda

Read More...

WATOTO 109,514 KUPATIWA CHANJO YA MATONE DHIDI YA POLIO WILAYANI NKASI MKOANI RUKWA

Katika utekelezaji wa zoezi la Kampeni ya chanjo ya matone dhidi ya ugonjwa wa  Polio, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu