Jeshi la Korea Kusini linasema kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio kombora lingine.

In Kimataifa

Jeshi la Korea Kusini linasema kuwa Korea Kaskazini imefanyia majaribio kombora lingine.

Ofisi ya kijeshi nchini Korea Kusini inasema kuwa kombora hilo lilirushwa siku ya Jumapili jioni saa za Korea.

Jaribio hilo linafanyika wiki moja baada ya Korea Kaskazini kulifanyia majaribio kombora lingine ambalo inadai kuwa ni jipya na ambalo lina uwezo wa kubeba silaha kubwa ya nuklia.

Jumatatu iliyopita baraza la usalama la Umoja wa Mataifa liliitaka Korea Kaskazinia kusitisha majaribio kama hayo.

Ulisisitiza umuhimu wa nchi hiyo kuachana na hatua hizo.

Korea Kaskania inafahamika kwa kuunda zana za nuklia na imefanya jumla ya jaribio matano ya nuklia na ya makombora yenye uwezo wa kosafirisha zana hizo hadi maeneo inayolenga.

Korea Kusini inasema kuwa jaribio la hivi punde lilifanyiwa eneo la Pukchang magharibi mwa nchi.

Join Our Newsletter!

Get updates, news etc from us. Its simple just put in your email address.

You may also read!

WANAFUNZI 500 WAPEWA MBINU WASILOWEE KWENYE MADAWA YA KULEVYA.

Na Tonie kaisoe ,Arusha Wanafunzi zaidi ya 500 wa shule ya Sekondari Arusha Jiji na Wilaya ya Arumeru wamepewa mbinu

Read More...

MR. IBU AFARIKI DUNIA

Mchekeshaji maarufu wa Nollywood nchini Nigeria, John Okafor, almaarufu Mr. Ibu amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Read More...

POLISI, LATRA WAPIGA FAINI MABASI YALIYO ZIDISHA NAULI ARUSHA.

Jeshi la Polisi kikosi cha Usalama Barabarani Mkoa wa Arusha kwa kushirikaiana na Mamlaka ya Udhibiti Usafiri Ardhini (LATRA)

Read More...

Leave a reply:

Your email address will not be published.

Mobile Sliding Menu